KARIBU MKURANGA

Thursday, March 1, 2012

KIKAO KATI YA BODI YA SHULE YA MWINYI SEKONDARI, MENEJIMENTI NA WA WAKILISHI WA MKURANGA NDIO KWETU

Assalaam Alyekum waukae,
Kwa niaba yangu binafsi, kwa niaba ya wana jumuiya ya Mkuranga NDIO Kwetu na kwa niaba ya wana Mkuranga wote napenda kuwa taarifu rasmi kikao cha Kesho tarehe 03/03/2012 baina ya Bodi ya shule ya Mwinyi Sekondari, Uongozi wa shule na wawakilishi wa wana jumuiya ya Mkuranga NDIO Kwetu. Lengo la kikao hicho ni kujadili changamoto za Elimu ( Kushuka Kiwango cha Ufaulu) na kujaribu kutafuta suluhisho ya changamoto hizo.

Pia tutajaribu kujadili uzoefu mdogo uliopatikana katika hamasa ya ya ELIMU zilizofanyika Mwinyi, Kiparang'anda na Lukanga Sekondari.

Mkuranga NDIO Kwetu itawakilishwa na
  1. Baraka Mwago
  2. Farida Mgomi
  3. Ramadhani Magimba
  4. Zawady Ally
  5. Rashid Selungwi 
  6. Hidaya Omari 
  7. Nyimgeni Mohamed 
Wote wenye ajenda yeyote inayodhaniwa ni muhimu jadiliwa ziwakilishwe kwa wa wakilishi wetu/wenu

Wasalaam,
Baraka Mwago
M/Kiti Mkuranga NDIO Kwetu

No comments:

Post a Comment