Wana wa Kwetu ni faraja kubwa kwangu kuwatangazia kuwa kesho tarehe 04/03/2012 tutazindua Kampeni ya Kufundisha kwa kujtolea kwa wanafunzi wote wa shule za Sekondari za Wilaya ya Mkuranga. Kituo cha kwanza ambacho kitakuwa cha tathimini (Pilot) kitakuwa Mwinyi Sekondari na baadae tutaanzisha vituo katika centers zingine kwa mgawanyiko wa Tarafa na hata Kata.
Programu hii itasimamiwa na kuendeshwa na Vijana wasomi wa wilaya ya Mkuranga kwa malengo makuu
Tunatanguliza shukrani kwako wewe mdau wa wilaya yetu nasi tunaona fahari kubwa Mkuranga kuwa Kwetu
Programu hii itasimamiwa na kuendeshwa na Vijana wasomi wa wilaya ya Mkuranga kwa malengo makuu
- Kuongeza kiwango cha ufaulu katika matokeo ya Kitaifa ya Kidato cha Pili na Nne
- Kujenga Hamasa kwa wanafunzi wa wilaya ya Mkuranga Kupenda kusoma na Kufaulu
- Vijana wasomi wa Mkuranga ikiwa ni sehemu yao ya ushiriki wa Maendeleo ya Nyumbani Kwao
- Vijana wasomi wazawa wa Mkuranga ikiwa ni sehemu ya kurudisha fadhila kwa rasilimali za Mkuranga zilizo wasomesha
Tunatanguliza shukrani kwako wewe mdau wa wilaya yetu nasi tunaona fahari kubwa Mkuranga kuwa Kwetu